Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China Bibi Hua Chunying amesema pande husika zinatakiwa kukumbuka lengo la mwanzo katika utatuzi wa suala la nyuklia la peninsula ya Korea
Bi Hua amesema hayo baada ya hivi karibuni rais wa zamani wa Marekani James Carter kuandika makala akisema kuna uwekezano wa kutokea tena kwa vita ya Korea, na Marekani inatakiwa kutoa pendekezo la kupeleka ujumbe kufanya mazungumzo ya amani na Korea Kaskazini au kufanya mkutano wa kimataifa utakaohudhuriwa na pande husika.
Bibi Hua Chunying amesema, kiini cha suala la nyuklia la peninsula ya Korea ni usalama. Pande husika zinatakiwa kutatua ufuatiliaji wa pande husika kwa uwiano, na kutafuta njia ya kutatua suala hilo kwa amani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |