Shirika la Fedha la Kimataifa IMF limepandisha makadirio yake kuhusu ongezeko la uchumi wa dunia katika mwaka huu na mwaka kesho kwa asilimia 0.1 na kufikia asilimia 3.6 na asilimia 3.7 mtawalia.
Jana, IMF ilitoa ripoti ya makadirio ya uchumi wa dunia ikikadiria kuwa asilimia 75 ya makundi ya uchumi duniani yatakua kwa kasi zaidi mwaka huu.
IMF pia limepandisha makadirio yake kuhusu ukuaji wa uchumi wa China katika mwaka huu na mwaka kesho kwa asilimia 0.1 na kufikia aslimia 6.8 na asilimia 6.5 mtawalia, ikiwa ni mara ya nne katika mwaka huu kwa IMF kupandisha makadirio yake kuhusu ukuaji wa uchumi wa China.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |