Wiki iliyopita, Jopo la waamuzi wa michezo nchini Kenya liliunga mkono uamuzi wa shirika la kukabiliana na matumizi ya dawa za kusisimua misuli la Kenya (ADAK) kuwa wanariadha hao walivunja sheria zinazopinga matumizi ya dawa hizo.
Shieys alipatikana na hatia ya kutumia dawa zilizoharamishwa baada ya vipimo wakati wa mbio za kilomita 21 za Hari Sukan Negara jijini Kuala Kumpur nchini Malaysia mnamo Oktoba 8, 2016. Naye Chepsoi alishiriki shindano moja nchini Uchina mnamo Novemba mwaka 2015 baada ya kupatikana na kosa la kutumia dawa zilizoharamishwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |