Makocha 28 wanawake kutoka vyuo mbalimbali vya maendeleo ya jamii nchini Tanzania wamehitimu kozi fupi ya ukocha katika kozi iliyoratibiwa kwa pamoja kati ya shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) na taasisi ya karibu Tanzania (KTO).
Kozi hiyo ya siku mbili ambayo ni ya pili kufanyika kwa makocha hao, iliyofanyika kwenye uwanja wa Karume - makao makuu ya TFF ilikuwa chini ya mkufunzi wa TFF, Raymond Gweba.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |