• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Betri mpya ya magari inahitaji kuchajiwa kwa dakika 6 tu

    (GMT+08:00) 2017-10-18 10:34:00

    Kampuni ya Toshiba ya Japan imesanifu betri mpya ya magari yenye ukubwa wa mkono ambayo inahitaji kuchajiwa kwa dakika 6 tu.

    Tofauti na betri nyingine za Li-ion ambazo ncha hasi zilitengenezwa na grafati, betri mpya imetengenezwa na Niobium Titanium Oxide, ambayo inaleta nishati nyingine na inaweza kuchajiwa kwa muda mfupi sana. Betri za kawaida za magari zikichajiwa kwa nusu saa umeme utafikia asilimia 80, lakini betri mpya ikichaji kwa dakika 6, umeme utafikia asilimia 90. Magari ya majaribio ya kampuni hiyo yalikwenda kilomita 320 baada ya kuchajiwa kwa dakika 6 tu.

    Aidha, betri mpya ikichajiwa na kutumiwa kwa mara 5000, bado ina zaidi ya asilimia 90 ya ujazo wa betri mpya, na inaweza kuchajiwa katika mazingira baridi yenye joto la nyuzi 10 chini ya sifuri sentigredi.

    Kampuni ya Toshiba itaendelea kuboresha betri hiyo, na kujaribu kuuza bidhaa rasmi ifikapo mwaka 2019.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako