Mchezaji wa tenis raia wa Uingereza, Heather Watson ametinga hatua ya robo fainali ya michuano ya wazi ya Luxembourg (Luxembourg Open) baada ya kumshinda mpinzani wake, Anett Kontaveit. Watson mwenye umri wa miaka 25, ametumia saa moja na sekunde 24 pekee kumfunga Anett Kontaveit kwa jumla ya seti 6-4 6-4. Muingereza huyo anaeshika nafasi ya pili katika viwango vya mchezo huo sasa atacheza na Elise Mertens.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |