• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Umoja wa Ulaya wapanga kurekebisha miji ya Ulaya kwa ajili ya kukinga mashambulizi ya kigaidi

    (GMT+08:00) 2017-10-19 09:44:32

    Kamishna wa kamati ya Umoja wa Ulaya anayeshughulikia mambo ya usalama Bw Jullian King amesema Umoja wa Ulaya utatumia Euro milioni 118.5 kuirekebisha baadhi ya miji barani Ulaya, ili kupunguza hatari ya kutokea kwa mashambulizi ya kigaidi.

    Bw Jullian amesema nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya zitaweka sera kali ili kuimarisha udhibiti wa uuzaji wa bidhaa za kemikali, na kujenga uwezo wa kukabiliana na matishio ya mashambulizi ya kikemikali, kibiolojia na kinyuklia.

    Amesema marekebisho hayo ni pamoja na kupanga upya sehemu za umma, taa na mifumo ya kukabiliana na hali ya dharura mijini, ili kuifanya miji hiyo iwe salama zaidi.

    Ameongeza kuwa jumuiya ya kimataifa bado inakabiliwa na changamoto kubwa katika kupamabana na ugaidi, na bado ipo uwezekano wa kutokea kwa mashambulizi ya kigaidi huko Ulaya.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako