Tume ya uchaguzi na kura za maoni ya jimbo la wakurdi nchini Iraq imesema kazi ya maandalizi ya uchaguzi wa wabunge na mwenyekiti jimbo la wakurdi uliopangwa kufanyika tarehe mosi mwezi ujao imesimamishwa, na upigaji kura wa uchaguzi huo utaahirishwa.
Taarifa iliyotolewa na tume hiyo imesema kutokana na hali ya wasiwasi kwenye jimbo hilo na kuchelewa kwa kazi ya kuandikisha wagombea, kazi ya maandalizi ya uchaguzi huo itasimamishwa hadi uamuzi mpya utakapotolewa na bunge la jimbo hilo.
Mwenyekiti wa jimbo la wakurdi Bw Massoud Barzani alisaini amri tarehe 19 mwezi Juni, akitoa agizo la kufanya uchaguzi wa wabunge na mwenyekiti Novemba mosi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |