Mshambuliaji Mganda Emmanuel Okwi jumamosi amefunga magoli 2 na kuseti 2 ambapo Simba ikiibuka na ushindi wa 4-0 dhidi ya Njombe Mji. Kwa ushindi huo, Simba imeendelea kukaa kileleni mwa ligi hiyo. Azam wao wakiwa ugenini wameambulia sare ya bila kufungana na Mbao fc, Mtibwa Sugar imeshinda goli 1-0 dhidi ya timu ngumu ya Prisons, nayo Lipuli ikiifunga Wanalizombe Majimaji goli 1-0. Yanga ikicheza uwanja wa nyumbani imepata ushindi wa goli 2-0 dhidi ya Stand United.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |