• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Utafiti waonesha kutia Lithium kwenye maji ya bomba kunaweza kukinga ugonjwa wa Alzheimer

    (GMT+08:00) 2017-10-23 08:58:25

    Wanasayansi wa Denmark wamefanya utafiti ukionesha kuwa, kutia Lithium kwenye maji ya bomba kunawaza kuwasaidia watu kukinga ugonjwa wa Alzheimer, ambayo itakuwa njia yenye gharama ya chini ya kukinga ugonjwa huo.

    Lithium ni aina ya chuma chenye rangi ya fedha, ambayo iko ndani ya njia ya bomba katika maji ya bomba. Utafiti wa awali umeonesha kuwa Lithium inaweza kutumiwa kutuliza hali ya moyo.

    Wanasayansi kutoka chuo kikuu cha Copenhagen wametoa ripoti ikisema, wamelinganisha kiwango cha ugonjwa wa Alzheimer katika baadhi ya sehemu nchini Denmark na kiwango cha lithium ndani ya maji ya bomba.

    Utafiti umeonesha kuwa, kiwango cha juu cha lithium katika njia ya bomba kinaweza kupunguza dhahiri kiwango cha ugonjwa wa Alzheimer.

    Watafiti wanaona kuwa kutia lithium kwenye maji kweli kunaweza kuwafanya watu wengi zaidi kuwa mbali na ugonjwa wa Alzheimer, lakini lithium hiyo inatakiwa kuwa katika kiwango mwafaka, kwa kuwa kiwango cha juu au cha chini kinaleta madhara.

    Wanasayansi wa Uingereza wamesema, kiwango cha lithium katika maji kina uhusiano wa wazi na ugonjwa wa Alzheimer, lakini hatuwezi kutia lithium ndani ya maji kabla ya kufahamu kiwango mwafaka.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako