Shirika la kuhudumia watoto la Umoja wa mataifa UNICEF limesema kutokana na hatua zinazochukuliwa sasa, itachukua zaidi ya miaka mia moja kutokomeza ndoa za utotoni katika eneo la Afrika magharibi na kati. Makadirio hayo mapya yaliyotolewa kwenye mkutano wa ngazi ya juu kuhusu kutokomeza ndoa za utotoni uliofanyika huko Dakar nchini Senegal wiki hii, yanalenga kuihimiza jumuiya ya kimataifa ifuatilie kanda hizo ambako wasichana wanakabiliwa na hatari kubwa ya kulazimishwa kuolewa wakiwa watoto.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |