• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Marekani na Russia zasisitiza Iraq itatue masuala yote kwa njia ya mazungumzo

    (GMT+08:00) 2017-10-24 09:43:09
    Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Bw. Rex Tillerson jana alipofanya mazungumzo na waziri mkuu wa Iraq Bw. Haider al-Abadi alisema Marekani inataka mazungumzo yafanyike kati ya serikali ya Iraq na jimbo la wakurdi ili kutatua mgogoro.

    Bw. Abadi amesema hatua zinazochukuliwa na serikali ya Iraq huko Kirkuk, ni kupanga upya na kutekeleza madaraka ya utawala, ambazo ni hatua halali kwa mujibu wa katiba na sheria, na kwamba serikali kuu haitaki kupambana na upande wowote wa Iraq.

    Habari nyingine zinasema waziri wa mambo ya nje wa Russia Bw. Sergey Lavrov jana huko Moscow alipokutana na waziri wa mambo ya nje wa Iraq Bw. Ibrahim al-Jaafari, alisema Russia inaheshimu ukamilifu wa ardhi wa Iraq na Russia inatoa wito wa masuala yote kutatuliwa kwa njia ya mazungumzo, pia alisistiza kuwa wakati wa kuhimiza utatuzi wa kisiasa wa migogoro ya kikanda, ni muhimu kuzuia kutenga au kuweka mipaka kwa kufuata dini au makabila.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako