Mfalme wa Morocco Mohammed wa Sita amewafuta kazi mawaziri wanne kutokana na kuchelewesha miradi ya maendeleo mjini Al Hoceima, kaskazini mashariki mwa nchi hiyo. Waliofukuzwa kazi ni mawaziri wa elimu, afya, mipango ya taifa na katibu anayeshughulikia mafunzo kazi. Mwaka 2015, Morocco ilizindua mradi mkubwa wa maendeleo mjini Al Hoceima, lakini programu nyingi zimeshindwa au kucheleweshwa kutokana na uzembe wa maofisa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |