Wizara ya afya ya Uganda imesema wafanyakazi wawili wa afya kwenye sehemu ya mashariki ya nchi hiyo wameonesha dalili za kuambukizwa virusi vya homa ya Marburg. Waziri wa afya wa nchi hiyo Bibi Jane Aceng amesema wafanyakazi hao walimshughulikia mgonjwa wa homa hiyo aliyefariki Oktoba 11 kwenye hospitali ya Kapchorwa, na hivi sasa wamewekwa kwenye karantini. Kwa mujibu wa waziri huyo, jumla ya watu 155 waliokuwa na mawasiliano ya karibu na mgonjwa huyo wanafuatiliwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |