• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • China yafanya juhudi kuhimiza kazi ya kujenga Jumuiya ya mustakabali wa pamoja wa binadamu

    (GMT+08:00) 2017-10-25 13:36:41

    Bw. Xi Jinping amesema, tangu Mkutano mkuu wa 19 wa Chama cha Kikomunisti cha China uanzishwe, vyama 452 vikubwa kutoka nchi 165 vimetuma barua 855 za pongezi, ambazo 814 zilitumwa na marais wa nchi, wakuu wa serikali, na viongozi wa vyama na mashirika muhimu. Anatoa shukrani za dhati kwa viongozi hao akiwa kwa niaba ya Kamati kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China. Bw. Xi amesema Chama cha Kikomunisti cha China na wananchi wa China waliwahi kukumbwa balaa na taabu kubwa, wanajua zaidi kuthamini amani na maendeleo. Wachina wanajiamini na kujiheshimu, watalinda kithabiti mamlaka ya nchi, usalama na maslahi ya maendeleo ya taifa lao, watajiunga na watu wa nchi mbalimbali kusukuma mbele ujenzi wa Jumuiya ya mustakabali wa pamoja wa binadamu, na watatoa mchango mpya mkubwa zaidi kwa mambo makubwa ya kutimiza amani na maendeleo ya binadamu.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako