Wizara ya afya ya Zambia imesema idadi ya watu walioambukizwa kipindupindu mjini Lusaka imeongezeka na kufikia 130 tangu mlipuko wa ugonjwa huo uibuke mwanzoni mwa mwezi huu. Ofisa habari wa wizara hiyo Bw Stanslous Ngosa amesema asilimia kubwa ya wagonjwa wametibiwa, na wizara hiyo inashirikiana na wadau kuboresha upatikanaji wa maji safi ya kunywa. Takwimu zinaonesha mpaka sasa ugonjwa huo umesababisha kifo cha mtu mmoja nchini humo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |