• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Marais wa China na Marekani waongea kwa njia ya simu

    (GMT+08:00) 2017-10-26 09:31:16
    Rais Xi Jinping wa China ameongea kwa njia ya simu na rais Donald Trump wa Marekani. Kwenye maongezi yao rais Trump amepongeza kufungwa kwa mafanikio kwa Mkutano mkuu wa 19 wa Chama cha Kikomunisti cha China, na kuchaguliwa tena kwa rais Xi kuwa katibu mkuu wa chama. Amesema ana matarajio kuhusu mazungumzo kati yake na rais Xi Jinping yatakayofanyika mjini Beijing, na kubadilishana naye maoni kuhusu kuimarisha ushirikiano kati ya pande hizo mbili, pamoja na masuala ya kimataifa na kikanda wanayofuatilia kwa pamoja.

    Kwa upande wake Rais Xi Jinping ametoa shukrani kwa salamu za pongezi za rais Trump, akisema China itashikilia njia ya kujiendeleza kwa amani, kuendelea kufuata mkakati wa kufungua mlango kwa nje, kupanua maslahi ya pamoja ya nchi mbalimbali, na kuhimiza uratibu na ushirikiano kati ya nchi mbalimbali.

    Rais Xi amesisitiza kuwa China inaweka mkazo mkubwa katika kukuza uhusiano na Marekani kwenye msingi wa kuheshimiana na kunufaishana.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako