Klabu ya Barcelona inataraji kubadili jina la uwanja wao wa sasa wa Nou Camp na kuwa "Nou Camp Grifol" jina ambalo litaanza kutumika katika msimu ujao wa ligi wa 2018/2018. Barcelona wamekubali kubadili jina hilo baada ya kusaini dili na kampuni inayohusiana na masuala ya dawa na kemikali iitwayo Grifol ambapo dili hilo linatajwa kuwa na thamani ya zaidi ya kiasi cha £340m.
Mkataba wa Grifol na Barcelona utawafanya Grifol kulipia marekebisho ya uwanja wa sasa wa Barcelona lakini vile vile mkataba huo wa Grifol unaweza kutumika katika mkataba mpya wa Lioneil Messi.
Dili hili linataraji kuwasaidia Barcelona katika mkataba mpya wa Lioneil Messi ambaye hadi sasa hajasaini kutokana na kiasi kikubwa cha pesa ambacho Messi anataka kupewa katika mkataba huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |