Tume ya kutoa misaada ya Umoja wa mataifa nchini Libya UNSMIL imetoa wito wa uchunguzi kufanyika haraka kuhusu mauaji ya watu 36 yaliyotokea karibu na mji wa Benghazi, mashariki mwa Libya, na kuwafikisha wahusika mbele ya sheria. Jumamosi Jeshi la taifa la Libya mashariki mwa nchi, lilitoa amri ya kufungua uchunguzi wa haraka kuhusu tukio hilo, baada ya miili ya watu 36 wenye majeraha ya risasi kugunduliwa kwenye eneo la Abyar, kilomita 50 kusini magharibi mwa Benghazi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |