Rais Donald Trump wa Marekani ametangaza kuwa jeshi la nchi hiyo limemkamata mshukiwa anayetuhumiwa kuhusika na shambulizi lililotokea Septemba 11 mwaka 2012 dhidi ya ubalozi mdogo wa Marekani mjini Benghazi, na kusababisha vifo vya raia wanne wa Marekani, akiwemo balozi wa Marekani nchini Libya. Kwenye taarifa yake rais Trump amesema kamwe Marekani haitasitisha msako dhidi ya wahusika wa shambulizi hilo, hadi watakapofikishwa mbele ya sheria.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |