Wanawake kuruhusiwa kuingia viwanja vya michezo Saudi Arabia
(GMT+08:00) 2017-10-31 08:47:55
Saudi Arabia itawaruhusu wanawake kuhudhuria michezo katika viwanja vya michezo kwa mara ya kwanza kuanzia mwaka ujao. Familia zitaweza kuingia kwenye viwanja 3 vya michezo vya Riyadh, Jeddah na Dammam.
Hii ni hatua nyingine ya kuwapa wanawake uhuru. Miezi michache iliyopita nchi hiyo iliruhusu wanawake kuendesha magari kwa mara ya kwanza.