Takwimu rasmi zinaonesha kuwa kiwango cha watu wasioajiriwa katika miji ya China kipo kwenye asilimia 3.95 hadi kufikia mwishoni mwa robo tatu ya mwaka huu, kikiwa kimeshuka sana tangu mwaka 2008.
Akitoa takwimu hizo afisa mwandamizi wa Wizara ya Rasilimali Watu na Usalama wa Jamii amesema, China imetoa ajira milioni 10.97 katika miezi tisa ya mwanzo, zikiongezeka laki 3 kuliko mwaka jana kipindi kama hiki. Soko la ajira linaendelea kuwa tulivu kukiwa na kiwango cha chini cha watu wasio na ajira tangu msukosuko wa fedha utokee mwaka 2008.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |