Waziri wa mambo ya nje wa Morocco Bw Naser Bourita, amefanya mazungumzo na katibu mkuu wa jumuiya ya nchi za Sahel na Sahara Bw Ibrahim Sani Abani, kuhusu matishio ya kiusalama yanayoikabili kanda hiyo. Viongozi hao wawili wametahadharisha kuhusu kuongezeka kwa ugaidi na uhalifu wa kimataifa wa kupangwa kwenye kanda hiyo. Baada ya mazungumzo hayo, Bw Abani amesema kuna haja ya kuimarisha haraka ushirikiano kati ya nchi za kikanda ili kukabiliana na matishio hayo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |