Waendesha mashtaka wa Marekani wamefungua mashtaka ya ugaidi dhidi ya mtuhumiwa wa shambulizi la kuwaparamia watu kwa lori dogo mjini New York, lililosababisha vifo vya watu nane na wengine wengi kujeruhiwa.
Kaimu mwanasheria wa Manhattan Bw. Joon Kim ametangaza mashtaka hayo kwenye mkutano na waandishi wa habari mjini New York.
Naibu mkurugenzi wa polisi wa New York John Miller amesema mtuhumiwa wa shambulizi hilo Bw Sayfullo Saipov amepanga shambulizi hilo la kigaidi kwa wiki kadhaa, ambalo alilitaja ni shambulizi kubwa mjini New York baada ya shambulizi lililotokea tarehe 11 Septemba mwaka 2011.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |