• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Baraza kuu la Umoja wa Mataifa lapitisha azimio la kuihimiza Marekani kuondoa vikwazo dhidi ya Cuba

    (GMT+08:00) 2017-11-02 18:43:40

    Mkutano wa 72 wa baraza kuu la Umoja wa Mataifa janaulipitisha azimio kwa kura nyingi ukiihimiza Marekani kuondoa vikwazo vya kiuchumi, kibiashara na fedha dhidi ya Cuba vilivyodumu kwa nusu karne.

    Mkutano huo uliupigia kura ya maoni mswada wa azimio linalosisitiza kuondoa vikwazo hivyo, na nchi zote 193 wanachama za Umoja wa Mataifa zilipiga kura na kupitisha azimio hilo kwa kura 191 za ndiyo na kura 2 za hapana. Marekani na Israel zilipiga kura za hapana.

    Azimio hilo lilizitaka nchi zote kutotoa au kutekeleza sheria na hatua za kuweka vikwazo dhidi ya Cuba, na kuzisisitiza nchi zinazoendelea na utaratibu huo kuchukua hatua mapema ya kuondoa vikwazo hivyo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako