Ofisi ya utendaji ya kuondoa mabomu ya ardhini ya Umoja wa Mataifa jana imetoa taarifa ikisema, zaidi ya watu milioni 6 nchini Sudan Kusini wanaishi kwenye sehemu inayotishiwa na mabomu ya ardhini na mabomu mengine yaliyobaki vitani.
Taarifa hiyo imesema, mabomu 150 ya aina mbalimbali yanagunduliwa kila mwezi nchini humo. Mabomu hayo si kama tu yamewazuia raia kukimbia kutoka sehemu ya migogoro, bali pia yamezuia msaada wa kibinadamu, vilevile yamezuia maendeleo ya jamii na uchumi nchini humo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |