• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tume ya Uchaguzi ya Libya yasaini makubaliano na UN kuunga mkono uchaguzi nchini humo

    (GMT+08:00) 2017-11-07 09:54:56

    Tume ya ngazi ya juu ya Uchaguzi ya Libya imeamua kusaini makubaliano kuhusu utoaji wa msaada wa ufundi na vifaa na Umoja wa Mataifa, ili kuunga mkono uchaguzi wa rais na wabunge utakaofanyika mwaka kesho nchini humo.

    Mkuu wa tume hiyo Bw. Imad Al-Sayah amesema kuwa tume hiyo inasubiri Ujumbe wa utoaji wa msaada wa Umoja wa Mataifa nchini Libya kukamilisha uratibu kati ya Libya na nchi zinazotoa msaada, kwa kuunga mkono uchaguzi utakaofanyika nchini humo.

    Pia amesisitiza kuwa Libya iko tayari kufanya uchaguzi ndani ya miezi minne tangu bunge la nchi hiyo lilipopitisha sheria ya uchaguzi.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako