• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Idadi ya watu waliofariki katika tetemeko la ardhi lililotokea kwenye mpaka kati ya Iran na Iraq yafikia 328

    (GMT+08:00) 2017-11-13 18:13:34

    Watu 328 wamefariki baada ya tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 7.3 kwenye kipimo cha Richter kutokea kwenye eneo la mpaka kati ya Iran na Iraq jana.

    Tetemeko hilo lililotokea kilomita 103 kusini mashariki mwa mji wa Sulaymaniyah, pia limesababisha watu wengine 4,000 kujeruhiwa. Zaidi ya vijiji 20 katika mkoa wa Kermanshah nchini Iran vimeathirika na huduma ya maji na umeme pia imekatika.

    Nchini Iraq, watu wanane wamefariki na mamia wengine kujeruhiwa katika tetemeko hilo. Idara ya usalama katika mji wa Sulaimaniyah kaskazini mashariki mwa Iraq imesema, idadi kubwa ya vifo imetokea kwenye mkoa unaojiendesha wa Kurdistan, ambapo watu saba wamefariki na wengine zaidi ya 300 kujeruhiwa.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako