• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ladumisha kuondoka kwa sehemu vikwazo vya silaha kwa Somalia kwa mwaka mmoja zaidi
     

    (GMT+08:00) 2017-11-15 18:13:56

    Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeongeza muda wa kuondoa kwa sehemu vikwazo vya kuiuzia silaha Somalia kwa mwaka mmoja zaidi.

    Baraza hilo lenye nchi wajumbe 15 lilipitisha Azimio namba 2385 la kuongeza muda huo kwa nchi za Somalia na Eritrea, ambapo nchi 11 zilipiga kura ya ndio huku Bolivia, China, Misri na Russia zikiacha kupiga kura hiyo. Baraza hilo pia limeongeza muda wa kikosi cha usimamizi katika nchi za Somalia na Eritrea mpaka mwisho wa mwaka ujao, na kutambua kuwa wakati wa majukumu yake ya sasa na yaliyopita, kikosi hicho kimeshindwa kupata ushahidi kamili kuwa Eritrea inaunga mkono kundi la Al Shabaab la Somalia.

    Akizungumzia hatua hiyo, naibu balozi wa China katika Umoja wa Mataifa Bw. Wu Haitao amesema, China haikupiga kura hiyo kwa sababu inaona kuwa azimio hilo linahitaji kufanyiwa maboresho kwani kuondoa vikwazo ni njia ya kusaidia kutatua masuala husika ya kikanda.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako