• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Rwanda: Vijana Rwanda watakiwa kuwa wabunifu

    (GMT+08:00) 2017-11-17 18:51:37
    Vijana nchini Rwanda wametakiwa kuwa wabunifu zaidi ili kujiongezea mgao wa soko la bidhaa mpya na kushindana kikamilifu.

    Mkuu wa kitengo cha utekelezaji wa miradi katika wizara ya vijana William Furaha pia amewataka vijana kutumia raslimali chache walizonazo kuanzisha biashara na pia kubuni bidhaa mpya.

    Furaha aliyasema hayo kwenye hafla ya YouthConnekt Awards kuzawadi vijana wabunifu kwenye eneo la Kaskazini.

    Mshindi wa tuzo hilo alikuwa ni Jean Paul Ntezimana, mwenye unmri wa miaka 26 anayezalisha mvinyo kwa kutumia viazi

    Ntezimana anamiliki kampuni ya mvinyo ya Iyiwacu Wine inazozalisha pia biskuti na donati kwa kutumia viazi.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako