Vikosi vya usalama vya Pakistan vimefanya operesheni mjini Quetta, kusini magharibi mwa nchi hiyo, baada ya makundi ya kigaidi kuongeza mashambulizi dhidi ya polisi na maofisa wa jeshi mjini humo. Operesheni hiyo ya siku moja imefanywa kutokana na taarifa za kiintelijinsia kuwa magaidi wamejificha kwenye eneo la Pashtoon Abad mjini humo. Ofisa mmoja wa jeshi amesema operesheni hiyo pia inalenga kutoa ujumbe kwa umma kwamba maofisa wa usalama wanadhamiria kuwaangamiza magaidi na kuhakikisha usalama wa wananchi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |