Jumla ya watoto wanane na wanawake watatu wameuawa baada ya shambulizi la anga lililoongozwa na Saudi Arabia kuharibu nyumba ya familia moja katika jimbo la Jawf kaskazini mwa Yemen. Wanaharakati kutoka jimbo hilo wamethibitisha idadi ya wahanga kwenye shambulizi hilo, ambalo ni jipya kati ya mashambulizi ya anga yanayofanywa na muungano unaoongozwa na Saudi Arabia, tangu vita ianze miaka miwili na nusu iliyopita.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |