Magoli mawili ya Mazembe ambao ndiyo mabingwa watetezi wa kombe hilo, yamefungwa na Adama Traore na Daniel Nii Adjei.
Lakini goli moja la kwa Supersport United lilifungwa na Sipho Mbule katika dakika arobaini na saba likiwa lenye umuhimu zaidi kuelekea mechi ya marudiano itakayoamua bingwa.
Mechi ya pili itafanyika Novemba 25 mjini Pretoria nchini Afrika Kusini.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |