Rais mteule wa Kenya Uhuru Kenyatta ameapishwa leo kuendelea kuiongoza nchi hiyo katika muhula wake wa pili madarakani katika sherehe zilizofanyika katika uwanja wa Kasarani jijini Nairobi na kuhudhuriwa na wageni kutoka nchi za nje na maelfu ya wafuasi wake.
Rais Kenyatta ameapishwa baada ya ushindi aliopata kwenye marudio ya uchaguzi wa rais uliofanyika Oktoba 26.
Hali ya usalama iliimarishwa ndani na nje ya uwanja huo, huku maofisa wa kijeshi wenye silaha nzito wakilinda eneo hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |