• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Anthony Joshua aongoza orodha ya wachezaji 12 wanaowania tuzo ya mwanamichezo bora wa mwaka 2017

    (GMT+08:00) 2017-11-29 09:06:27

    Bingwa wa uzito wa juu duniani, Anthony Joshua anaongoza katika orodha ya wachezaji 12 waliotangazwa kuwania tuzo ya mwanamichezo bora wa mwaka 2017 nchini Uingereza kupitia shirika la BBC. Joshua mwenye umri wa miaka 28, ambae ni bingwa wa zamani wa Olympic na bingwa wa uzito wa juu amekuwa akipendwa zaidi tangu alipotwaa taji lake la WBA na IBO baada ya kumshinda mpinzani wake Wladimir Klitschko katika dimba la Wembley mwezi Aprili.

    Bondia huyo alifanikiwa kuutetea mkanda wake wa IBF katika pambano lake la hivi karibuni dhidi ya Carlos Takam mwezi Oktoba katika Uwanja wa Cardiff Principality..

    Anthony Joshua anakabiliana na ushindani mkubwa kutoka kwa bingwa wa mwaka 2014, Lewis Hamilton ambae pia ni mshindi mara nne wa mashindano ya Formula One na Chris Froome mshindi mara nne wa mashindano ya Tour de France

    Pia orodha hiyo imejumuisha mwanariadha, Mo Farah mshindi wa mbio za dunia mita 10,000 jijini London na mchezaji wa Tottenham, Harry Kane. Naye mchezaji tenis namba moja kwa ubora nchini Uingereza, Johanna Konta ni miongoni mwa wachezaji waliotangazwa katika orodha ya kuwania kinyang'anyiro hicho.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako