• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Rais mpya wa Zimbabwe atangaza baraza jipya la mawaziri

    (GMT+08:00) 2017-12-01 20:00:45

    Rais Emmerson Mnangagwa wa Zimbabwe ameteua baraza jipya la mawaziri lenye watu 22, wengi wao wakitoka chama tawala cha ZANU-PF.

    Rais Mnangagwa amemteua Sibusiso Moyo kuwa waziri wa mambo ya nje, Perence Shiri kuwa waziri wa ardhi na utamaduni, Patrick Chinamasa ameteuliwa kuwa waziri wa fedha, Christopher Mutsvangwa kuwa waziri wa habari. Wengine walioteuliwa ni Obert Mpofu kuwa waziri wa mambo ya ndani, Kembo Mohadi kuwa waziri wa ulinzi na Ziyambi Ziyambi kuwa waziri wa sheria.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako