Katibu mkuu wa chama tawala cha Jubilee nchini Kenya Bw. Raphael Tuju jana hapa Beijing amesema, China imetoa misaada mingi kwa Kenya katika kutimiza lengo la maendeleo ya viwanda, na chama cha Jubilee kinataka kuiga uzoefu wa ujenzi wa chama cha siasa kutoka kwa Chama cha Kikomunisti cha China CPC, ili kuongoza Kenya kupata maendeleo ya kasi zaidi.
Bw. Tuju amesema, chama cha Jubilee cha Kenya kinapenda kujifunza kutoka CPC kuhusu namna ya kubadilisha mawazo, na kutunga mpango wa maendeleo ya muda mrefu na ya katikati, ili kukabiliana na masuala mapya na changamoto mpya.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |