• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Katibu mkuu wa UM alaani mauaji ya walinzi wa amani nchini Afrika ya kati

    (GMT+08:00) 2017-12-05 09:22:12

    Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Antonio Guterres amelaani shambulizi dhidi ya kituo cha ukaguzi cha polisi wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR, ambapo askari mmoja wa kulinda amani ameuawa na wengine watatu wamejeruhiwa.

    Msemaji wa katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Stephane Dujarric, amesema shambulizi hilo lilifanywa na wapiganaji wa anti-Balaka mjini Baria, na kusababisha kifo cha askari mmoja kutoka Mauritania.

    Shambulizi hilo lilitokea saa mbili baada ya askari wa kulinda amani kuingilia kati kuwakomboa wakimbizi wawili waliotekwa nyara na wapiganaji wa anti-Balaka mjini Baria.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako