Chama tawala nchini Afrika Kusini ANC kimemchagua Bw. Cyril Ramaphosa kuwa mwenyekiti wa chama hicho kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.
Bw. Ramaphosa ambaye ni naibu rais wa nchi hiyo alipambana vikali na aliyekuwa mwenyekiti wa kamati ya Umoja wa Afrika Bibi Nkosazana Dlamini Zuma kugombea nafasi ya uenyekiti wa ANC. Ushindi huo wa Bw. Ramaphosa umewafurahisha wataalam ambao wanaamini kuwa kiongozi huyo mpya atahamasisha imani ya masoko na wawekezaji.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |