Rais Xi Jinping wa China amempigia simu rais Rodrigo Duterte wa Philippines, na kutoa salamu za pole kwa vifo, mejeruhi na hasara ya mali zilizosababishwa na dhoruba ya Tembin, na kusema China iko tayari kutoa msaada wa uokoaji kama ikihitajika.
Dhoruba ya Tembin ilikishambulia kisiwa cha Mindanao nchini Philippines, na kusababisha mafuriko ya ghafla na maporomoko ya udongo katika eneo hilo. Mpaka sasa idadi ya watu waliofariki kutokana na dhoruba hiyo imefikia 200, wengine 159 hawajulikani walipo, na watu zaidi 70,000 wamepoteza makazi yao.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |