• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Carlos Carvalhal kuwa kocha mpya wa Swansea City

    (GMT+08:00) 2017-12-29 08:39:53

    Swansea City wamemteua aliyekuwa mkufunzi wa klabu ya Sheffield Wednesday Carlos Carvalhal kuwa mkufunzi mpya. Kocha mchezaji Leon Britton alikuwa akisimamia Swansea kwa muda tangu klabu hiyo iliyopo chini ya msimamo wa ligi imfute kazi Paul Clement tarehe 20 Disemba.

    Carvalhal, mwenye mika 52, alitimuliwa kazini na klabu ya Wednesday mkesha wa siku ya krisimasi huku klabu hiyo ya daraja la kwanza ikiwa katika nafasi ya 15 katika msimamo wa daraja la kwanza. Raia huyo wa Ureno anajiunga na Swansea hadi mwisho wa msimu akiwa na fursa ya kuongeza mkataba huo. Carvalhal ambaye ni mkufunzi wa tano wa Swansea katika kipindi cha miaka miwili, aliongoza Wednesday kufika katika raundi ya muondoano katika misimu miwili ilopita.

    Mkufunzi huyo wa zamani wa klabu ya Besikitas, Sporting Lisbon na Maritimo ambaye alirithi nafasi ya Stuart Gray huko Hillsborough mwezi Juni 2015 alifanikiwa kupata ushindi wa asilimia 42.7 katika mechi zake 131 alizosimamia.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako