Rais Bashar al-Assad wa Syria ameamua kufanya mabadiliko katika baraza la mawaziri na kuwabadilisha mawaziri wa ulinzi, habari na viwanda. Rais Assad amemteua mnadhimu mkuu wa jeshi Jenerali Ali Abdullah Ayyoub kuwa waziri mpya wa ulinzi, mkurugenzi wa televisheni ya taifa Emad Sara kuwa waziri mpya wa habari, na Bw. Muhammad Mazen Ali Youssef ameteuliwa kuwa waziri mpya wa viwanda.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |