• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Man City waendelea kuchanja mbuga ligi Kuu England

    (GMT+08:00) 2018-01-04 10:35:26
    Ligi Kuu England msimu wa 2017/2018 imeendelea tena usiku wa January 3 2018 kwa mchezo mmoja wa London Derby kuchezwa katika uwanja wa Emirates kati ya wenyeji Arsenal dhidi ya Chelsea huku timu zote zikiwa zinatoka jiji la London na kufanya mvuto wa mchezo huu uwe mkubwa.

    Arsenal wakiwa nyumbani licha ya kuongoza kwa kumiliki mpira kwa asilimia 58 dhidi ya asimilia 42 ya Chelsea wamejikuta wakilazimishwa sare ya magoli 2-2. magoli ya Arsenal yakifungwa na Jack Wilshere dakika ya 63 na Hector Bellerin dakika ya 90. Kwa upande wa Chelsea magoli yao yalifungwa na Eden Hazard kwa penati dakika ya 67 na Marcos Alonso dakika ya 84, sare hiyo sasa inaifanya Chelsea kushuka nafasi ya tatu katika msimamo wa Ligi kwa kufikisha jumla ya point 46.

    Nafasi ya pili wapo Man United wana point 47 huku Man City wao wakijikita kileleni kwa kuwa na jumla ya point 62 tofauti ya point 15 na Man United wanaowafuatia, Arsenal wameshuka hadi nafasi ya sita wakiwa na jumla ya point 39.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako