Wizara ya mambo ya nje ya Marekani imetangaza kuwa, serikali ya nchi hiyo imesitisha msaada wa usalama wa dola za kimarekani bilioni 255 kwa Pakistan.
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani Bi. Heather Nauert amesema, msaada huo utarejeshwa pale Pakistan itakapochukua hatua zenye uamuzi za kupambana makundi likiwemo kundi la Taliban nchini Afghanistan na mtandao wa kundi la Haqqani ambalo Marekani imeliweka kwenye orodha ya makundi ya kigaidi.
Hii ni mara ya pili kwa Marekani kusitisha msaada wa fedha kwa Pakistan ndani ya miezi sita.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |