Waganda wanaoishi na kufanya kazi nje ya nchi wamekumbushwa kuwekeza katika nchi yao ili kuchangia mapato ya chi.
Kwa mujibu wa takwimu za benki ya Uganda ushuru unaoingia katika akaunti zao kutoka nje umefikia dola bilioni 1 ambazo ni zaidi ya dola milioni 600 zinazotoka kwa misaada .
Wataalamu wanasema fedha hizo kutoka nje zimekuwa kwa asilimia 21 katika mda wa miaka 5 iliyopita na zinachangia pakubwa uchumi wa Uganda.
Sasa wanauchumi pamoja na wizara ya fedha ya nchi hiyo imewataka waganda hao kutumia fdeha zao kuwekeza nchini humo ili zizalishe mapato zaidi ya kiuchumi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |