Akizungumza baada ya kumaliza kwa ajenda zote za mkutano wa ngazi ya juu kati ya Korea Kusini na Korea Kaskazini, naibu waziri wa mawasiliano wa Korea Kusini anayeshughulikia masuala ya peninsula ya Korea Bw. Chun Hae-sung amesema, nchi yake imependekeza ushirikiano na Korea Kaskazini wakati wa ufunguzi wa michezo hiyo.
Pia Korea Kusini imependekeza kufanya hafla ya kuungana tena kwa familia katika sikukuu ya Spring, na kufanya mkutano wa mashirika ya Msalaba Mwekundu na ya kijeshi ili kuzuia mapambano
Kwa upande wake, Korea Kaskazini imekubali kutuma ujumbe wa Kamati ya Taifa ya Olimpiki, wachezaji, washangiliaji, timu ya sanaa, timu ya maonyesho ya utamaduni wa Taekwondo, watalii na waandishi wa habari kushiriki kwenye michezo hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |