• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Rwanda: MTN Rwanda yaungana na Vanu

    (GMT+08:00) 2018-01-09 19:28:09

    Watu zaidi nchini Rwanda wanatarajiwa kupata huduma bora za mawasiliano ya simu za rununu baada ya kampuni mbili za mawasiliano MTN na Vanu kuungana.

    Kufuatia muungano huo wa kibiashara, sasa huduma za GSM kama vile kupiga simu na data hasa kwenye maeneo ya vijijini yataweza kuwa na huduma bora.

    Hatua hii haitasaidia tu wateja wa MTN lakini pia na kufungua fursa ya ukuaji kwa kampuni hiyo.

    Mkurugenzi wa Vanu Rwanda Anthony Masozera amesema pia muungano huo utawezesha wateja kufurahia huduma ya kutuma na kupokea simu kwa njia ya simu.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako