Watu watatu wameuawa katika shambulizi lililofanywa mkoa wa Far North nchini Cameroon, huku kundi la Boko Haram likishukiwa kuhusika na shambulizi hilo.
Shambulizi hilo limetokea kata ya Kolofata kaskazini mwa nchi hiyo, ikiwa ni mpakani na kambi ya kundi hilo nchini Nigeria. Shambulizi hilo linahisiwa kuhusika na juhudi za kundi la Boko Haram kuiba chakula kutoka kwa wakazi wa eneo hilo kutokana na taarifa kuwa akiba yao ya chakula inakaribia kumalizika.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |