• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Umoja wa Mataifa waonesha wasiwasi juu ya watu waliozingirwa nchini Syria

    (GMT+08:00) 2018-01-12 10:00:46

    Naibu Katibu mkuu wa umoja wa mataifa anayeshughulikia mambo ya kibinadamu Bw. Mark Lowcock ,ameeleza wasiwasi juu ya hali ya raia waliozingirwa kwenye sehemu ya Ghouta Mashariki, kitongoji cha mji Damascus, pamoja na maeneo mengine yenye mgogoro nchini Syria.

    Bw Lowcook amesema, anafuatilia hali ya watu waliozingirwa kwenye sehemu ya Ghouta Mashariki inayokaliwa na wapiganaji, ambako mapambano kati ya jeshi la serikali na wapiganaji yamekuwa yakipamba moto.

    Ofisa huyo pia amefanya mazungumzo ya wazi na serikali ya Syria kuhusu mgogoro huo na jinsi inavyopunguza hali ya wasiwasi wa kibinadamu.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako