Jeshi la Uganda limelaani shambulizi lililofanywa na waasi wa kundi la ADF dhidi ya jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (FARDC), na kusababisha vifo vya askari watatu na wengine watano kujeruhiwa.
Msemaji wa jeshi la Uganda Bw. Richard Karemire amesema, kitendo hicho cha ADF hakitazuia jitihada za kikanda za kuliondoa kundi hilo. Jeshi la Uganda UPDF litaendelea kushirikiana na jeshi la serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kuwafukuza wale wanaovuruga amani ya ya kikanda.
Habari zinasema, waasi wa ADF walishambulia kambi ya jeshi la serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ya Muzambay katika jimbo la Kivu Kaskazini baada kufukuzwa na jeshi la Uganda.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |